Tuesday, April 23, 2013

Pratap Ghose atangazwa Mkurugenzi Mtendaji mpya Zantel



Mkurugenzi Mkuu mpya wa Zantel, Pratap Ghose akizungumza na waandishi wa habari hivi karibuni
Dar es Salaam-April 22,2013: Kampuni ya simu za mikononi ya Zantel imemteua na kumtangaza, Pratap Ghose, kuwa Mkurugenzi Mtendaji mpya wa Zantel Tanzania.
Kabla ya uteuzi huu, Pratap ambaye ana miaka 18 ya uzoefu kwenye sekta mbalimbali ikiwemo mawasiliano alikuwa makamu wa Rais wa Etisalat, Uchumi na ukuzaji wa biashara kwa kanda ya Afrika.

Pratap anachukua nafasi ya Ali Bin Jarsh ambaye ameiongoza Zantel kwa miaka miwili na kuipatia mafanikio makubwa.
Bwana Pratap pia ameshikilia nafasi mbalimbali ikiwemo Afsa fedha mkuu wa kampuni dada ya Etisalat, India pamoja na kuwa mjumbe wa bodi ya wakurugenzi wa kampuni ya Atlantique kanda ya Afrika magharibi.

Pratap pia ana uzoefu mkubwa wa soko la Tanzania akiwa amefanya kazi kama mshauri wa Zantel na pia kwa kipndi cha miaka miwili alikuwa Afsa fedha mkuu wa TIGO Tanzania.

Ikizungumzia uteuzi wake, Zantel Tanzania imesema imefurahishwa na ujio wa bwana Pratap kwani uzoefu wake kutoka nchi za India, Nigeria pamoja na Mashariki ya Kati utaipeleka mbali kampuni yao.

Pratap ana shahada ya juu katika biashara kutoka chuo cha biashara cha Melbourne na pia ni mhasibu aliyebobea. Akiwa Zantel, Pratap atakuwa na jukumu la kuongeza idadi ya wateja, pamoja na kusimamia ukuaji wa kampuni na vyanzo tofauti vya mapato.

Pratap Ghose akibadilishana mawazo na Prof. John Nkoma wa TCRA walipokutana hivi karibuni

No comments:

Post a Comment